Burudani

Mark Zuckerberg alijibu ombi la Kanye West la kuwekeza $1bn kwenye idea zake

Mwanzilishi na CEO wa Facebook, Mark Zuckerberg hajamtafuta Kanye West kama ambavyo rapper huyo aliimba, lakini amemjibu kwa njia nyingine isiyo ya moja kwa moja.

mark-zuckerberg-microphone-2015-billboard-650

Kanye alimtaka bilionea huyo amsaidie kwa kuwekeza dola bilioni 1 kwenye idea zake anazoamini zitaubadilisha ulimwengu.

Zuckerberg hajajibu kwa maneno yake mwenyewe lakini alioesha kuwa anafahamu ombi la Kanye kwa kulike status ya Facebook ya mtumiaji wa mtandao huo.

44a955e8a4eeafabfdc1f12f64d099b8

Steven Grim aliandika kwenye mtandao huo, “Dear Kanye West: If you’re going to ask the CEO of Facebook for a billion dollars, maybe don’t do it on Twitter.”
Zuckerberg aliilike status hiyo.

Hii ni ishara kuwa Mark amelikaushia ombi la Kanye.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents