Burudani
Mastaa 10 wanaoingiza pesa nyingi kwa kupost tangazo Instagram
Instagram sio tena sehemu ya kupost picha pekee kwaajili ya kuuza sura kama zamani, mtandao huyo kwa sasa unawaingizia pesa nyingi baadhi ya mastaa duniani.
Staa wa soka Cristiano Ronaldo na muimbaji Selena Gomez na Kim Kardashian ndio mastaa pekee wanaolipwa pesa nyingi kwa post moja ya tangazo instagram.
Selena ambaye ni namba moja analipwa pound 425400 ambazo ni zaidi ya Tsh Bilioni 1.2, kwa upande wa Ronaldo ambaye ni namba tatu analipwa pound 309382 ambazo ni zaidi ya Tsh milioni 800.