Msanii wa vichekesho na muigizaji wa filamu nchini Maulid Ally aka ‘Mau Fundi,’ amesema kwa sasa huwa anapata nyimbo nyingi ili azirudie lakini hufanya parody (video za utani) anazozipenda tu.
Mau ameiambia Bongo5, “Unajua huwa natumiwa nyingi sana na wasanii wananiomba nizifanyie kazi lakini huwa nafanya hadi nyimbo nikiipenda na pia nitakuwa nafanya video nyingi tu ambazo mashabiki wangu watakuwa wanafurahi kwa kufanya na nyimbo za wasanii wa nje zikinikalia vizuri nitazibutua. Unajua Ulaya nyimbo za watu hizo, ila sasa hivi kuna project yangu naandaa kwahiyo mashabiki wangu wategemee tu kazi zinakuja.”
Angalia parody alizofanya msanii huyo ukiwemo wimbo wa Nuh Mziwanda na Bado ya Harmonize.
https://youtu.be/cVvpTQ6tNeA
https://youtu.be/XKmGjqwwcks