Burudani

Mr Ibu aliyefariki March 2 kuzikwa Juni 28

Marehemu muigizaji kutoka nchini Nigeria John Okafor (62) maarufu kama Mr Ibu anatarajiwa kuzikwa Juni 28, 2024.

Taarifa hiyo imetolewa na kaka mkubwa wa Mr Ibu Sunday Okafor ambapo ameeleza kuwa wameamua kuchelewesha mazishi hayo ili Mwigizaji huyo aweze kupewa mazishi ya kihistoria ambapo atazikwa nyumbani kwake katika mji aliozaliwa wa Amuri katika eneo la Serikali ya mtaa Nkanu Magharibi katika Jimbo la Enugu.

Kufuatia taarifa hiyo muongozaji wa mazishi hayo Mhe. Monday Diamond Ani ameweka wazi kuwa kutakuwa na sherehe ya siku tano ambapo hafla itaanza Juni 25 kutakuwa na mechi maalumu, Juni 26 Usiku wa Mr Ibu ambapo kutakuwa na mishumaa pamoja na kupata burudani ya moja kwa moja.

June 27 kutakuwa na ibada maalumu nyumbani kwao huko Eziokwe Amuri, huku Ibada ya mazishi ikifanyika June 28 na sherehe hizo zitatamatika Jumapili June 30 ambapo familia itatoa Shukrani kwa Kanisa, Marafiki na watu wengine waliohudhuria hafla zote za siku tano.

Ikumbukwe kuwa Mr Ibu (62) alifariki Dunia Machi 2, 2024 wakati akiendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Evercare iliyopo nchini Nigeria.

Mr Ibu watu Wengi walimtambua kupitia filamu zake kama The Collaborator, My Chop Money na nyingine nyingi akiwa na “Aki” na “Ukwa”.

 

 

 

 

 

 

 

Imeandikwa na Mbanga B.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents