Burudani

Nandy atoa fedha mfukoni kununua wimbo

Msanii wa muziki wa Bongo Flava, Nandy amesema wimbo wake mpya ‘Kivuruge’ ameununua.


Muimbaji huyo ambaye bado anafanya vizuri na ngoma ‘Wasikundanye’ ameiambia Dj Show ya Radio One kutokana ngoma hiyo alinunua hivyo wale wanaosema wimbo huo amemuimbia mtu fulani wanakosea.

“Kivuruge hapana!!, sijamuimbia mtu kabisa, siyo true story ni wimbo ambao nimekuta umeshatungwa, mwenye wimbo anaitwa J Melody ambaye yupo pale THT alikuwa amesharekodi kila kitu then nilivyoisikia nikaipenda nikamwambia aniuzie, then akaniuzia ikiwa kama ilivyo” amesema Nandy.

Kivuruge ni ngoma ya pili kwa Nandy kutoa kwa mwezi huu mara baada ya kutoa ngoma ‘Mahabuba’ aliyomshirikisha Aslay.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents