Burudani
Ne-Yo atua Uganda, atatumbuiza Ijumaa hii
Muimbaji wa Marekani, Ne-Yo ametua jijini Kampala, Uganda kwaajili ya show yake Ijumaa hii kwenye uwanja wa cricket wa Lugogo.
Hiyo ni mara ya kwanza kwa muimbaji huyo wa ‘Closer’ kwenda nchini Uganda, lakini mara ya tatu Afrika.
Ni hivi karibuni tu muimbaji huyo alikuwa nchini Kenya kurekodi na wasanii mbalimbali kwenye kipindi cha Coke Studio Africa.
Baada ya kutua Kampala, muimbaji huyo alipost picha na kuandika: Waddup Uganda…..”