Burudani
New Singles Alert: Izzo B, Shaa, Madee na Damian Soul kuja na zao (Picha)
Wakati mfungo wa Ramadhan ukiendelea, wasanii mbalimbali wameendelea kuandaa silaha zao kuziachia katika kipindi hiki.
July 4, Shaa ataachia single yake mpya iitwayo ‘Subira’ huku Madee akijiandaa kuachia yake ‘Sheeda’ iliyotayarishwa na Marco Chali.
Rapper wa Mbeya, Izzo Bizness pia ataachia yake iitwayo ‘Walala Hoi’ na Damian Soul ataachia yake iitwayo Dua la Kuku aliyomshirikisha Banana Zorro.