Burudani
Ngoma ya ‘Bodak Yellow’ ya Cardi B yavunja rekodi Billboard
Rapper Cardi B amekuwa wa kwanza kwa takribani miaka 19 kwa kutinga nafasi ya kwanza katika chati za muziki za Billboard Hot 100 bila kollabo.
Cardi B ameweka rekodi hiyo kupitia ngoma yake ya ‘Bodak Yellow’ mwaka 1998 Lauryn Hill ndiyo alikuwa ameshika nafasi hiyo kupitia ngoma ya Doo Wop (That Thing).
Mrembo mwenye asili ya Latini ambaye amekuwa tishio kwa marapper wa kike kama Nick Minaj ameweka rekodi hiyo Septemba 25, 2017 kwenye chati hizo mama za muziki Marekani na kwa kuitoa ngoma ‘Look what you made me do’ ya mwanadada Taylor Swift.
Cardi B alikuwa akishika namba mbili kwa muda mrefu kabla ya kuongoza na pia ni msanii wa Latina kuongoza chati hiyo toka mwaka 2006 ambapo Shakira aliwakilisha kupitia ‘Hips Don’t Lie’.