Michezo
Pablo Franco: Sisi ndiyo Mabingwa wa michuno hii
Kocha wa Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Azam Sports Federation na Mapinduzi Cup Simba SC, Pablo Franco amesema kuwa watahakikisha wanafanikiwa kulitetea taji lao la michuano ya ASFC kwa kuwafunga Ruvu Shooting hapo kesho.
”Sisi ndiyo Mabingwa wa michuano hii na malengo yetu ni kuhakikisha tunavuka hatua na kwenda robo fainali na hatimaye tulitetee kombe letu.” – Kocha wa klabu ya Simba Pablo
Simba itashuka katika uwanja wa Benjamin Mkapa hapo kesho siku ya Jumatano ya Februari 16, 2022 kuwakabili vijana wa Masau Bwire, Ruvu Shooting mchezo wa raundi ya 16 Bora.