Picha: Mgahawa mpya ‘VVK’ wa Khadija Mwanamboka wazinduliwa jijini Dar
Mbunifu wa mavazi, Khadija Mwanamboka amezindua mgahawa mpya uitwao VVK pamoja na super market itakayokuwa inatoa huduma ya chakula cha aina mbalimbali pamoja na kuandaa events.
Mteja akifanya shopping ndani ya VVK Super Market
Akizungumza na Bongo5 jana Kinondoni jijini Dar es salaam, Khadija alisema mgahawa huo pia utakuwa unasambaza chakula kwa order maalum kwa wateja watakaohitaji.
Baadhi ya wadau wakipata chakula
“Siku za wiki tutatoa namba za simu halafu wateja wanapiga simu na uletewa chakula kwa gharama ndogo utakayolipia lakini weekend Ijumaa, Jumamosi na Jumapili kutakuwa kuna bufee, yaani mtu anaweza akajipakulia mwenyewe chakula kwa gharama nafuu. Na chakula ni cha kiswahili, wali, ugali, mboga za majani ni vya asili,” amesema Khadija.
Asia Idarous akiwa ndani ya VVK
“Halafu vile vile kuna super market hapa ambayo tumeweka kashata za kila aina tuna mboga mboga za wakulima wa Lushoto, tuna matunda mbalimbali, mafenesi yakiwa kwenye makopo mazuri unapewa na umma unaweza ukala hata kwenye gari. Pia unaweza kupata chakula kwa njia mbili, kuna application inaitwa ‘Hellofood’ ipo kwenye play store unaweza ukai-store kwenye simu yako halafu ikifungua utakuta migahawa mingi, utautafuta VVK ambao ndio huu, ukifunguka utakuta huduma za vyakula tulivyokuwa navyo. Sasa pale ndo unaweza kuchagua chakula unachotaka na sisi tutakuletea.”
“Huduma zingine unaweza ukatupigia sisi wenyewe VVK kama unataka chakula au kwaajili ya event kwa namba 0755551077 utahudumiwa. Sisi tupo block 41 nyuma ya jengo la Airtel, mtaa unaitwa Maji Street ni mtaa wa kwanza kushoto baada ya Dawasco.”
Asia Idarous na mdau wake wakiwa ndani ya VVK
Shamim Mwasha akipata fresh juice