Picha
Picha: Peter Okoye(P-Square) apata mtoto wa kike
Peter Okoye wa kundi la P-Square na mke wake jana wamebahatika kupata mtoto wa pili wa kike waliyempa jina ‘Aliona’. Mtoto huyo amezaliwa huko San Francisco nchini Marekani ambako Peter yupo nchini humo kwa mapumziko na familia yake.
Amezibreak good news hizo kwa kuweka picha kwenye mtandao wa Instagram akiwa hospitali bega kwa bega na mke wake ambapo kwenye picha hiyo ya juu ameandika,”Thank u Lord… Am the new Daddy in town…. And she is so beautiful and adorable.”
Peter ana mtoto mwingine wa kiume aitwaye Cameron.