Habari

Picha: Rais Magufuli aongoza kuagwa kwa mwili wa marehemu Joseph Mungai

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk John Pombe Magufuli amewaongoza waombolezaji kuaga mwili wa marehemu Joseph Mungai kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam, Alhamis hii.

mmg_4006

Msiba huo umehudhuriwa na viongozi wengine wa serikali akiwemo Rais wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa, Jaji Joseph Warioba, Dk Augustine Mahiga, William Lukuvi, Fredrick Sumaye Steven Wasira, Mama Salma Kikwete, Makamu wa Rais Mstaafu, Mohamed Gharib Bilal na wengine.

Mungai aliwahi kuwa Mbunge wa jimbo la Mufindi Kaskazini Mkoani Iringa lakini pia aliwahi kuwa Waziri katika wizara mbalimbali kuanzia serikali ya awamu ya kwanza ya Mwalimu Nyerere hadi ile ya awamu ya nne ya Jakaya Kikwete. Atazikwa Ijumaa hii nyumbani kwao Mufindi.

mmg_4037-copy

mmg_4064

mmg_4085

mmg_4106

Picha na Michuzi

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents