Habari

Prof. Ndalichako awasimamisha kazi vigogo wawili

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako amewasimamisha kazi Kaimu Kamishna wa Elimu, Nicholas Bureta na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu ya Tanzania, Dr. Elia Kidga kufuatia sakata la kasoro zilizopo katika vitabu vya kujifunzia wanafunzi.

Prof. Ndalichako ametangaza kuwasimamisha kazi watu hao kufuatia mjadala uliobika bungeni kuhusu kasoro kwenye vitabu hivyo ambavyo vimechapishwa na taasisi hiyo kwa ajili ya kufundishia.

“Kwa mamlaka niliyonayo, ninamuagiza Kaimu Kamishna wa Elimu na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania, kuondoka ofisini mara moja ili kupisha uchunguzi,” alisema Ndalichako

Waziri Ndalichako amewasimamisha viongozi hao na ameliambia bunge kuwa uchunguzi wa kina unafanyika na baada ya kukamilika hatua za kinidhamu na kisheria zitachukuliwa dhidi ya wote waliohusika.

Na Emmy Mwaipopo

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents