Burudani
Rapper maarufu nchini Marekani apagawishwa na ngoma ya Tetema ya Rayvanny Ft Diamond (+video)
Rapper maarufu nchini Marekani, Kevin Gates amekunwa na ngoma mpya ya TETEMA ya msanii wa Bongo Fleva, Rayvanny .
Kevin Gates ambaye alishawahi kutamba na ngoma kibao ikiwemo ‘Out The Mud’ ameposti kipande cha video kwenye ukurasa wake wa Instagram, akisikiliza ngoma ya Tetema.
Wimbo wa Tetema ni moja ya nyimbo zinazosikilizwa sana mtandaoni kwa sasa nchini Tanzania, na tayari video ya wimbo huo imeshafikisha views milioni 2+ ndani ya siku tatu, tangu video hiyo iwekwe kwenye mtandao wa YouTube.