Burudani
Ray C kuanzisha ‘Ray C Foundation’, itakayoelimisha kuhusu madhara ya madawa ya kulevya
Baada ya kujiondoa kutoka kwenye utumiaji wa madawa ya kulevya na kurejea kwenye afya yake, Rehema Chalamila aka Ray C ameanzisha taasisi yake itakayokuwa ikitoa elimu kuhusiana na madhara ya utumiaji wa madawa ya kulevya.
Kupitia Instagram Ray C aliandika: Asante wapenzi nataka kusaidia jamii yangu ijue madhara ya madawa ya kulevya,walioathirika watoke Kama mimi na ambao hawajawahi kamwe wasi thubutu ndio target yangu!!!!!Mungu Ana sababu na mimi na ndio mana aliniokoa.”
Ray C alisaidiwa na Rais Jakaya Kikwete kutoka kwenye janga hilo ambaye aligharamikia matibabu yake hadi alipopona.