MichezoUncategorized
Sijutii Chelsea kumuuza Mohamed Salah – Antonio Conte
Meneja wa klabu ya Chelsea, Antonio Conte amejitapa kuwa kamwe hajutii kitendo kilichofanywa na uongozi wa timu hiyo kumuuza mshambuliaji wao, Mohamed Salah mwaka 2014.
Salah mwenye umri wa miaka 25, ameondoka kwa mkopo Stamford Bridge Januari mwaka 2014 kisha rasmi mwaka 2016 wakati huo huo ambao Conte anajiunga na klabu hiyo na kusema kuwa halikuwa chaguo lake.
Hakuna mtu aliyeniuliza kuhusu yeye kwahiyo sihitaji kuhusishwa katika hili maana ningelikuwa kwenyematatizo.
Nadhani msimu huu ni bora mno kwa Salah, hapa tunazungumzia mchezaji bora. Nilimjulia Italia lakini msimu huu ulikuwa mgumu kutabiri.