Burudani

Sina mahusiano ya kimapenzi na Nay wa Mitego – NINI

Msanii wa muziki Bongo, Nini amefunguka kuhusu ukaribu wake na Nay wa Mitego.

Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na ngoma ‘Niwe Dawa’ alioshirikiana na Nay ameiambia The Playlist ya Times Fm kuwa hajawahi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na rapper huyo.

Kauli ya Nini anakuja baada ya hapo awali kuwepo taarifa kuwa sababu ya kutimuliwa MJ Record ni kuwa na mahusiano na Nay.

“Sina mahusiano ya kimapenzi na Nay, halafu hata kama ningekuwa nayo, kiupande wangu I don’t real think hiyo ni sababu ambayo ingeweza kumfanya yeye afanye kile alichokifanya,” amesema.

“Seriously sidhani kama mahusiano ya kimapenzi yanaweza kuathiri muziki, sina uhakika may be according to me navyofikiria lakini sidhani kama hiyo it can be specific reason,” amesisitiza.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents