Burudani
Tango TV yazindua application ya kutazama filamu za Kiswahili
Muda kidogo uliopita tuliandika story kuhusu kampuni mpya ya kitanzania iliyounda kifaa cha kutazama filamu kwenye TV kwa kutumia mtandao.
https://www.youtube.com/watch?v=x-hykniUF0M
Kampuni hiyo ilianza kuchukua orders za king’amuzi chao hicho ingawa bado hakijaanza kupatikana mtaani.
Lakini wiki hii tu wamezindua application ya simu za android ambayo in mamia ya filamu za kibongo.
“Natoa wito kwa watanzania waijaribu application hii ya Tango Movies, inapatikana kwenye playstore bure kabisa, install sasa upata offer ya kutazama filamu hizo bure,” amesema Victor Joseph ambaye ni Mkurugenzi wa Tango TV.
Itafute ufurahie filamu kibao za kibongo kupitia simu yako.