BurudaniUncategorized

‘Waka’ ya Diamond Platnumz yaweka rekodi mpya Afrika Mashariki

Wakati wimbo mpya wa Diamond Platnumz aliomshirikisha Rapper Rick Ross kutoka Marekani unatoka haukuwa na nguvu kubwa pengine kutokana na kuahirishwa kwa tarehe iliyotakiwa kutoka video ya wimbo.

Lakini hiyo haikuwa kigezo kikubwa kwa wimbo huo wa ‘Waka’ kwani ndani ya siku tatu ulikuwa tayari umefikisha views milioni 1.

Ukweli ni kwamba ‘Waka’ ulipata mapokezi ya kawaida ukilinganisha na nyimbo nyingine za Diamond Platnumz kama Hallelujah, Salome, Kidogo n.k , Lakini kitu cha kushangaza wimbo huo kadri siku zinavyozidi kwenda ndio unazidi kutazamwa zaidi sio tu Tanzania bali na nchi nyingine za Afrika Mashariki.

Kwa sasa wimbo wa ‘Waka’ unaweka rekodi ya kuwa wimbo wa kwanza kutrend namba moja kwa nchi tatu za Afrika Mashariki kwenye mtandao wa YouTube.

Video hiyo mpaka jana usiku ilikuwa ndiyo video inayotazamwa zaidi mtandaoni (Trending) kwa kushika namba moja kwa nchi za Kenya, Uganda na Tanzania.

Wimbo wa ‘Waka’ awali ulipotoka ulikaa siku mbili kwenye mtandao wa YouTube hapa Tanzania  bila kukaa kwenye namba 1 ya video zinazotrend hapa nchini. Lakini mpaka sasa video ya wimbo huo yenye siku saba mtandaoni ipo namba moja kwenye Trending.

Awali rekodi ya video iliyotrend namba 1 kwa nchi mbili tofauti tofauti ilikuwa ilikuwa inashikiliwa na video ya wimbo wa ‘Zilipendwa’ wa WCB , Salome ya Diamond Platnumz na Video ya wimbo wa ‘Seduce Me’ wa Alikiba ambapo video zote wakati zinatoka zilishika namba moja Tanzania na Kenya kwa muda tofauti tofauti.

 

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents