Tragedy

Westgate: Mpwa wa Rais Uhuru Kenyatta alipigwa risasi 8 baada ya kumkinga mchumba wake aliyeuawa pia

Mtoto wa binamu yake na Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya, Mbugua Mwangi ambaye ni miongoni mwa watu waliouawa na magaidi kwenye shambulio la mall ya Westgate jijini Nairobi, anadaiwa alipigwa risasi 8 baada ya kumkinga mchumba wake Rosemary Wahito dhidi ya magaidi hao.

0007e673-642
Mbugua na Rosemary walienda Westgate kununua pete za ndoa tayari kwa maandalizi ya harusi yao

Taarifa zinadai kuwa Mbugua na mchumba wake walikuwa wameenda kwenye mall hiyo kufanya shopping ya pete za ndoa, siku chache tu baada ya kuzitaarifu familia zao kuhusu mipango yao ya ndoa. Kwa mujibu taarifa hiyo, Mbugua alikuwa tayari ameshatoka nje baada ya magaidi hao kuishambulia mall hiyo na alipogundua kuwa mchumba wake alikuwa bado ndani alirudi kumuokoa na kukutana na na mauti hayo.

4_Mbugua_Mwangi
Mbugua aliuawa katika harakati za kumlinda mchumba wake

Kwa mujibu wa mashuhuda, wapenzi hao walikuwa pamoja pindi magaidi hao waliokuwa na silaha kali walipowaona, na Mbugua alimkingia kifua mchumba wake na hivyo kupigwa risasi 8 za moto. Wote waliuawa.

Mbugua alikuwa mtoto wa Catherine Mwangi (balozi wa zamani wa Kenya nchini Ireland) ambaye ni dada wa seneta Beth Mugo na mwanasiasa wa zamani Ngengi Muigai ambao ni mabinamu wa Rais Uhuru Kenyatta.

True Love….

Source: Niaje.com

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents