Habari

WHO imesema haiungi mkono baadhi ya nchi kuwaondoa wananchi wao China kisa Corona

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema WHO haiungi mkono baadhi ya Nchi kuwaondoa Wananchi wao China ili kuepuka maambukizi ya Virusi vya Corona.

“WHO ina imani China ina uwezo mkubwa wa kuzuia na kudhibiti maambukizi hayo” Taarifa hiyo imeeleza.

Kauli ya WHO inakuja kufuatia Japan na Marekani kuwaondoa Raia wao waliokuwa Wuhan eneo ambalo virusi hivyo vilianzia na Watu wengi kuathirika zaidi.

Idadi ya Watu waliofariki kwa Virusi vya Corona imefikia 132 China huku wagonjwa waliothibitishwa kuwa na Virusi hivyo wakifikia 5974.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents