Yanga Bongo Movie V Simba Bongo Movie
Timu ya wasanii wa filamu waliamua kujigawanya katika mafungu mawili, ya Simba na Yanga ilikuweza kukamilisha mazoezi ambayo ndani yake yalikuwa na kikombe. Lengo la mazoezi hayo ni kujiandaa na kandanda ambalo watakuja kucheza na Wabunge siku ya jumamosi ijayo, huko Dodoma.
Katika mechi hiyo wadau wa Bongo MovieMama Rupia, na Mussa ambao walitoa mchango wao na kufikia zaidi ya milioni2, papo kwa hapo kwaajili ya maandalizi mazima ya safari hiyo.
Katika mechi hiyo, timu ambayo wakereketwa wa Simba yaani Simba Bongo Movie, iliibuka na mabao mawili yaliyoingizwa nyavuni na Hassabi Kiduku, na bao la kufutia machozi lilifungwa na Vicent Kigosi maarufu kama Ray kwa mkwaju wa penati.
Ray na Cloud 112 wakisikiliza mawaidha ya kocha, baada ya kipindi cha kwanza kufungwa.
Wema Sepetu akiwa amemkalia Jack Wplper, na pembeni yao ni Janert ‘Odama’ wakisikiliza maneno ya kocha
Ray akipokea mkono kutoka kwa mgeni, baada ya kufungwa timu yao na kuwa washindi wa pili
Steven Kanumba yeye anasema alijua kama watafungwa, hivyo aliamua kujificha nyuma ya mti na kuangalia mpira kwa kuchungulia, huku akijikinga na jua.
Baada ya mpira kuisha, wasanii wote walikusanyaika sehemu moja, kwaajili ya kusikiliza maelezo kutoka kwa viongozi wa filamu Tanzania maarufu kama Bongo Movie, Chiki, Steven Nyerere, Cloud na wengine kwaajili ya maandalizi ya safari.
Hapa mshabiki wa kweli na kiongozi na mdau wa Yanga Sport Club, Kate akiishabikia timu yake ya Yanga Bongo Movie, huku akipuliziwa Vuvuzela.