Shamsa Ford aeleza jinsi alivyokutana na Chidi Mapenzi
Unakumbuka wewe na mpenzi wako mlikutana wapi mpaka mkaanzisha mahusiano?. Malkia wa filamu Shamsa Ford ameweka wazi jinsi alivyokutana na mpenzi wake mpaka wakafikia hatua ya kufunga ndoa hivi karibuni.
Shamsa Ford na mume wake
Mwigizaji huyo ambaye amefunga ndoa Ijumaa iliyopita na mfanyabiashara wa maduka ya nguo Chidi Mapenzi, amesema chakula ndiyo chanzo cha kukutana na mpenzi wake huyo.
“Siri ya mahusiano aijuae ni Mungu, nilikuwa napita tu ofisini kwako tena bila hata salamu. Nakumbuka siku niliyokuwa nakula karibu na ofisini kwako kwa bahati mbaya chakula kilinimwagikia kwenye nguo na ikanibidi niingie ofisini kwako ili niweze kununua nguo mpya.Dah kumbe Mungu alikuwa ananikutanisha na mume wangu kipenzi jamani. asante Mungu kwa mume bora uliyenipa. Muda wa Mungu ndio muda sahihi,” aliandika Shamsa instagram.
Katika ujumbe mwingine aliandika “Asante Mungu kwa kuweza kutusimamia kuweza kufanikisha shughuli yetu. Asante sana my mama yangu kipenzi, Asanteni sana familia ya MR Ford kwa kuwa na mimi bega kwa bega. Asante sana ndugu yangu kipenzi Zamaradi Mketema, Asanteni sana wasanii wenzangu wa Tasnia ya Wanawake kwa mchango mkubwa mlionionesha jana, Asanteni sana kaka zangu from bongo movie , Asante sana sana my dady Jimmy Mafufu, Asanteni sana marafiki zangu wote mlionionesha upendo kwa siku ya jana. Bila kusahau mashabiki zangu. Nawapenda na kuwaheshimu sana. Mungu atubariki sote.
Harusi hiyo ilifanyika Ijumaa iliyopita Sinza Afrikasana nyumbani kwa wazazi wa Shamsa na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali pamoja na wasanii wa filamu.