Habari

Virusi Vya Corona: Kisa cha kwanza cha Corona Afrika chathibitishwa Misri

Virusi Vya Corona: Kisa cha kwanza cha Corona Afrika chathibitishwa Misri

Wizara ya afya ya Misri imetangaza kisa cha kwanza kilichothibitishwa cha mgonjwa wa virusi vya Corona kinachokuwa cha kwanza pia barani Afrika.

Taarifa iliyotolewa na wizara hiyo imesema mgonjwa aliyebainika siyo raia wa Misri lakini pia haikufafanua uraia wa mtu huyo.

Maafisa wa Misri walifanikiwa kuthibutisha kisa hicho kupitia mpango ulioanzishwa na serikali wa kuwafuatilia abiria waliowasili kutoka nchini ambazo virusi vya Corona tayari vimesambaa.

Msemaji wa wizara ya afya ya Misri, Khaled Megahed, amesema serikali imechukua hatua za tahadhari na inafuatilia kwa karibu afya ya mgonjwa huyo ambayo imeripotiwa kuwa imara.

Mamlaka za Misri pia zimeliarifu shirika la afya duniani WHO kuhusiana na kisa hicho na tangu wakati huo mgonjwa huyo amewekwa karantini katika hospitali maalum ya umma.

Mapema mwezi huu Misri ilifuta safari zote za ndege za shirika la ndege ya taifa kwenda China. Na hatua hiyo itaendelea hadi mwishoni mwa mwezi huu.

Raia 301 na moja wa Misri waliondolewa kutoka mji wa Wuhan, kitovu cha mripuko huo wa virusi nchini China na tangu walipowasili wamewekwa karantini ya siku 14.

Mahusiano ya karibu na China na mifumo dhaifu ya afya ni masuala yanayozua wasiwasi kuhusu uwezo wa nchi za Afrika wa kukabilina na mripuko wa virusi vya Corona vinavyyowauwa maelfu ya watu nchini China.

 

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents