Michezo

16 bora ya ligi ya mabingwa kuanza wikiendi

Klabu ya  Mamelodi Sundowns Mabingwa wa klabu bingwa Afrika 2016

Hatua ya 16 bora ya michuano ya klabu bingwa Afrika inatarajiwa kuanza kutimua vumbi wikiendi hii katika hatua ya makundi, takribani michezo mitano itachezwa siku ya Ijumaa na mbili zikichezwa siku ya Jumamosi na moja kuchezwa Jumapili.

Mabingwa watetezi wa klabu bingwa Afrika, klabu ya Mamelodi Sundowns ya Afrika kusini itaanza kutetea taji lake Jumapili hii wakiwa wenyeji katika mchezo utakao chezwa dhidi ya Ethiopia.


Kocha wa Mamelodi Sundowns Pitso Mosimane

Kocha wa klabu hiyo, Pitso Mosimane amesema wana hofu ya kutetea taji lao kutokana na timu zote kuwa imara
Mwaka jana walikuwa katika nafasi ya pili katika klabu zenye ushindani nchini Afrika Kusini baada ya ushindi wake wa magoli 3 kwa 1 dhdid ya Zamalek ya Egypt katika mchezo wa fainali.
Mosimane, ambaye alishawahi kucheza Afrika kusini pamoja na kuwa kocha nchini humo amesema ratiba ya timu yake inaweza kuathiri timu yake

BY HAMZA FUMO

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents