Burudani

Picha/Video: Rayvanny alivyoitembeza tuzo yake ya BET mitaani leo

Leo mchana kwenye majira ya saa tisa, msanii Rayvanny aliwasili nchini akiwa na tuzo yake ya BET ambayo aliinyakuwa usiku wa Jumamosi nchini Marekani aliwasili katika uwanja wa JK. Nyerere na kupata mapokezi makubwa kama ya kifalme.

Hitmaker huyo wa Mbeleko alipokelewa katika uwanja huo na mabosi wake wa WCB wakiongozwa na Diamond, Mkubwa Fella, Sallam pamoja na wasanii wenzake akiwemo Harmonize, Rich Mavoko, Queen Darleen na Lava Lava walioambatana na Bi. Sandra ambaye ni mama mzazi wa Diamond.

Msanii huyo aliongozwa na msafara mkubwa pamoja na mashabiki wake na kuanza kuitembeza tuzo hiyo katika mitaa mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam, ikiwemo Buguruni, Kariakoo, Magomeni, Tandale, Sinza na Mikocheni.

Salum Kaorata na Laila Sued

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents