Burudani
Picha ya Oprah na Reese Witherspoon kwenye jarida la Vanity Fair yazua mshtuko
Picha iliyopigwa kwa ajili ya jarida la Vanity Fair imewashtua mashabiki wengi baada ya kumuonyesha Oprah Winfrey akionekana akiwa na mikono mitatu huku muigizaji Reese Witherspoon akionekana akiwa na miguu mitatu.
Baada ya mshtuko huo, Witherspoon aliandika ujumbe kwenye mtandao wake unaosomeka, “Well…I guess everybody knows now…I have 3 legs. I hope you can still accept me for who I am. π( and I will never apologize for snuggling @Oprah .. if you get the opportunity, I highly recommend it;).”
Hata hivyo Oprah alicomment kwenye ujumbe huo kwa kuandika, “I accept your 3d leg. As I know you accept my 3d handππΎππΎππΎβ€οΈ.”