Michezo

QPR yamtimua kocha wake, Ian Holloway

Meneja wa klabu ya Queens Park Rangers, Ian Holloway ameachishwa kazi ndani ya timu hiyo ya nchini Uingereza.

Holloway mwenye umri wa miaka 55 amejiunga na QPR Mwezi Novemba mwaka 2016 kwa dili la miaka miwili na nusu.

Hata hivyo, Holloway ameitumikia klabu hiyo kwa miezi 12 huku muda wake wa mkataba ukiwa bado wakati timu yake ikimaliza nafasi ya 16 kwenye msimamo wa ligi ya Championship ya Uingereza.

Kocha huyo wa zamani wa klabu ya Crystal Palace amekiongoza kikosi hicho katika michezo 80 huku akipoteza nusu yake.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents