Habari
Rais Trump atangaza tarehe na mahali atakapokutana na hasimu wake Kim Jon-Un
Rais wa Marekani, Donald Trump ametangaza tarehe na mahali ambapo atakutana na kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jon-Un.
Rais Trump ametangaza kupitia ukurasa wake wa Twitter, amesema atakutana na Kim Jong-un nchini Singapore mnamo tarehe 12 Juni mwaka huu.
The highly anticipated meeting between Kim Jong Un and myself will take place in Singapore on June 12th. We will both try to make it a very special moment for World Peace!
— Donald J. Trump (@realDonaldTrump) May 10, 2018
Trump mwezi Aprili mwaka huu alitangaza kuwa atakutana na kiongozi huyo jambo ambalo watu wengi hawakuamini kutokana na marumbano ya marais hao kwa muda mrefu.