Michezo
Hatima Ya Beckham kutojulikana
Mchezaji nyota wa klabu ya soccer ya Marekani L.A Galaxy, David Beckham anatarajia kumaliza mkataba wake na timu yake mwezi ujao, walakini kutokujulikana anakohamia kuendeleza fani yake hii ya mpira.
Beckham ambaye amebarikiwa mtoto wa kike kwa mkewe Victoria miezi michache iliyopita, ameweka wazi kwamba anaipenda Marekani, hasa mji wanaoishi huko California, na hivyo basi watapenda kuendelea kuishi huko kulea watoto wao.
Becks ambaye amewahi kuichezea timu ya Manchester United pamoja na Real Madrid inasemekana anaweza akahamia nchini Ufaransa kwenye timu ya Paris St Germain. Mpaka sasa Beckham hajazungumzia muafaka wake, lakini inawzekana sana akabaki na L.A Galaxy kwa mwaka mmoja zaidi.