Burudani
RC Makonda amkaribisha Waziri Mkuu Fiesta Dar ‘Njoo ule bata kidogo’ (+video)
Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam, Mhe. Paul Makonda amemualika Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa aje Dar kutazama kilele cha tamasha la Fiesta litakalofanyika mkoani humo katika Uwanja wa Taifa.
RC Makonda amesema kuwa Dar ndio mkoa wa Burudani Tanzania kwani matamasha yote makubwa yanafanyika mkoani humo, Ikiwemo Wasafi Festival na Muziki Mnene.