Michezo
Floyd Mayweather kuzichapa na Marcos Maidana, May 3
Bingwa wa mkanda wa WBC (welterweight) Floyd Mayweather atazichapa na bingwa wa mkanda wa WBA, Marcos Maidana May 3.
Bondia huyo wa Argentina amempiku Amir Khan wa Uingereza aliyekuwa anawania kuzichapa na Mayweather.
Madaina
Pambano la mwisho la Mayweather (45-0, 26 KO) lilikuwa September 14 mwaka jana alipochuana na Canelo Alvarez.