Picha: Uzinduzi wa video mbili za Professor Jay
Gwiji wa muziki wa Hip Hop Bongo, Joseph Haule aka Professor Jay usiku wa Jumamosi aliwapa zawadi mashabiki na wapenzi wa muziki wake kwa kwenye uzinduzi wa video zake mbili mpya, Tatu Chafu na Kipi Sijasikia. Uzinduzi huo ulifanyika ndani ya ukumbi wa Ten Lounge zamani ukifahamika kama Letasi Lounge uliopo maeneo ya Victoria jijini Dar. Wasanii wengine waliokuwepo ni pamoja na Chidi Benz,Wakazi,Soggy Doggy,Linex,Lady Jaydee,,Dogo Janja,Stara Thomas na TID.
Hizi ni picha za uzinduzi huo.
Lady Jaydee akiwasabahi mashabiki zake
Linex na Wakazi
M2 The P akiwa na Q Chilla
Msanii wa Bongo Movie, Tausi naye alikuwepo
Producer Lamar na Gadner G Habash
Producer Lamar na msanii wake Nuru
Professor Jay alipokuwa akiingia ukumbini
Professor Jay akizindua video zake
Stara Thomas katika pozi
TID ndo alikuwa MC, ilikuwa nomaa
Wema Sepetu na team yake