Gareth Southgate awatetea wachezaji wa Man United Chris Smalling na Luke Shaw
Gareth Southgate amabye ni kocha wa muda wa timu ya Uingereza amewatetea wachezaji wa Manchester United Chris Smalling na Luke Shaw, baada ya wao kulaumiwa na Meneja Jose Maurinho.
Mourinho aliwalaumu wachezaji hao kwa kukosa mechi ya Jamapili ambapo United walishinda Swansea mabao 3-1 akisema kuwa wangefanya vyovyote vile kuichezea timu hiyo.
Smalling ana jeraha la mguu naye Shaw alicheza mechi ya Alhamis ambapo Manchester United ilishindwa na klabu ya Fenerbahce.
Sasa Southgate anasema kuwa huenda kuna tatizo linalowakumba wachezaji hao wawili.
Smalling ambaye ana umri wa miaka 26 na Shaw 21, wameachwa nje ya kikosi cha Uingereza ambacho kitashiriki mechi ya kufuzu kwa kombe la dunia mwaka 2018 dhidi ya Scotland na mechi ya kirafiki ya wiki ijayo dhidi ya Uhispania.
Shaw amecheza mechi sita za ligi msimu huu tangu apone jeraha la mguu mwezi Septemba.