Idris Sultan adai Trevor Noah ni level ya juu kwake
Baada ya kukosa nafasi ya kuhost kwenye tuzo za MTV MAMA 2016, Idris Sultan amemfagilia mchekeshaji wa Afrika Kusini anayefanyika kazi nchini Marekani, Trevor Noah baada ya kuchaguliwa wenye nafasi hiyo.
Kupitia mtandao wake wa Instagram, Idris ameandika, “I would ‘ve never thought of a better host for MAMAs than my brother @trevornoah .Looking forward to the awesomest show @mtvbaseafrica ????????????.”
Awali Idris Sultan, Basket Mouth (Nigeria), Idris Elba (Uingereza) na Kevin Hart (Marekani) walikuwa miongoni mwa washereheshaji wengine waliokuwa wanawania nafasi hiyo.
Tuzo hizo zinatarajiwa kufanyika Oktoba 22 kwenye ukumbi wa Ticket Pro Dome, Johannesburg, Afrika Kusini huku wasanii kadhaa akiwemo Yemi Alade, Ycee, Cassper Nyovest, Alikiba na wengine wanatarajiwa kutumbuiza kwenye tuzo hizo.