Habari

Marekani kuikabidhi kambi yake ya anga ya Bagram kwa Afghanistan

Jeshi la Marekani litakabidhi kambi yake kuu ya anga ya Bagram kwa vikosi vya Afghanistan, huku ikiendelea na kuondoa askari wake wa mwisho nchini humo.

US to hand Bagram base to Afghan forces in 20 days, says official

Kambi hiyo iliyojengwa na Wasovieti katika miaka ya 1980, ndiyo kubwa zaidi na ikitumiwa na vikosi vya Marekani na jumuia ya kujihami ya NATO huko Afghanistan.

Afisa usalama wa Afghanistan alisema makabidhiano hayo yanatarajiwa kufanyika katika siku 20 zijazo na wizara ya ulinzi imeunda kamati maalum za kuisimamia.

The U.S. War in Afghanistan | Council on Foreign Relations

Kambi hiyo ambayo imekuwa ndiyo kituo kikuu cha kitaifa cha shughuli za jeshi la anga kwa miongo miwili iliyopita, kina gereza ambalo lilikuwa na maelfu ya wafungwa wa kundi la Taliban na wapiganaji wa jihadi.

Marekani tayari imekabidhi kambi nyingine kadhaa za kijeshi kwa vikosi vya Afghanistan kabla ya Mei 1, wakati ilipoanza kuharakisha mchakato wa kuwaondoa wanajeshi wake.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents