Siasa
Mbunge wa Kilombero Aboubakari Assenga, apiga magoti kwenye matope akiomba ujunzi wa barabara (+ Video)
Mbunge wa Jimbo la kilombero Aboubakari Assenga amelazimika Kupiga magoti kwa unyenyekevu kuiangukia wizara ya Ujenzi na kuiomba iweke mkazo kwenye Ujenzi wa barabara ya Ifakara hadi Kidatu ambayo imeharibika vibaya kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha Mkoani Morogoro.
Mvua hizo zimepelekea Mto Lumemo ambao ni mojawapo ya mito maarufu Katika eneo hilo kufurika na kusababisha mafuriko ambayo yamezuia kero kubwa.