Burudani
Morocco: Rapper, Gnawi ahukumiwa kwenda jela kwa kosa la kuwatusi Polisi
Rapper Mohamed Mounir maarufu ‘Gnawi’ amehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela kwa kosa la kutukana Polisi kupitia kipande cha video alichoposti kwenye mitandao ya kijamii.
Hata hivyo rapper huyo mwenye umri wa miaka 31, inadaiwa kuwa kukamatwa kwake kumechochewa zaidi na aina ya kazi zake za muziki, hata baada ya kuachia wimbo wake mpya ujilikanao kama “Aach al Chaab,” aliyowashirikisha Lz3er na Weld L’Griya ambao unazungumzia vitendo vya rushwa Serikalini.