Msanii mwingine wa Kenya asainishwa na Chocolate City ya Nigeria
Uongozi wa lebo ya Chocolate City umemsaini msanii mwingine kutoka nchini Kenya.
Lebo hiyo inayomilikiwa na rapper, M.I imetangaza kumsaini Eric Onyango Omollo maarufu kama Qritiqal na kumfanya kuwa msanii wa pili kutoka Kenya kusainiwa na lebo hiyo baada ya Victoria Kimani aliyesainiwa na lebo hiyo miaka mine iliyopita.
Kupitia akaunti ya instagram ya lebo hiyo wameandika:
Welcome to the family @Qritiqals! Chocolate City Kenya’s new signee is about to blow your minds. Follow him on Instagram, Twitter & FB – @Qritiqals.
Get ready Africa, it’s about to get Qritiqal. #WelcomeQritiqal #HelloQritiqal
Qritiqal amewahi kuachi nyimbo kadhaa ikiwemo ‘Chaguo Langu’ lakini pia amewahi kushirikishwa na rapper Colonel Mustafa kwenye wimbo wake wa ‘Kupe’.