Uncategorized
Mtanzania Shaaban Idd Chilunda apata shavu kwenye klabu nyingine ya nchini Hispania
Nyota wa Tanzania, Shaban IDD Chilunda hapo jana alitambulishwa rasimi kuwa mchezaji wa klabu ya CD Izarra inyoshiriki ligi daraja la pili nchini Hispania.
Chilunda amejiunga na klabu hiyo ya CD Izarra akitokea timu ya CD Tenerife inayoshiriki ligi daraja la kwanza ya nchini humo kwa usajili wa mkopo.
Chilunda ambaye alitokea Azam FC ya jijini Dar es Salaam alijiunga na CD Tenerife kwa msimu wa mwaka 2018/19.