Picha
Nje ya Box: H.Baba atengeneza pipi za watoto, zina ladha ya maziwa
Wakati wasanii mbalimbali nchini wakiendelea kubuni shughuli mbalimbali za ujasiriamali tofauti na kutegemea muziki, hitmaker wa Mpenzi Bubu, H.Baba amefikiria nje ya box na kuanzisha pipi za watoto zenye jina lake.
Pipi hizo zinazotengenezwa na kampuni ya TANFRIK LIMITED ya Nairobi nchini Kenya, zinaitwa ‘H. Baba & Flora Mapenzi kwa Watoto’.
“Nimeanzisha biashara ya pipi za watoto zina maziwa tamu balaa.Siku ya Jumamosi ntashow love na mashabiki wangu pale round about ya Samaki, ntaganda kama sanamu la samaki kuanzia saa 10 jioni mpaka saa 1 usiku pia ntagawa pipi za H.Baba hapa jijini Mwanza,” ameimbia Bongo5.
Msikilize zaidi hapa kama alivyozungumza na blog ya G Sengo ya Mwanza.
PICHA: gsengo.blogspot.com