Michezo
Pambano la Mayweather na Pacquiao huenda likapigwa Dubai, 2015
Pambano la masumbwi linalosubiriwa kwa hamu kati ya Floyd Mayweather na Manny Pacquiao linaweza kupigwa Mashariki ya Kati.
Ripoti zinadai kuwa kundi la wawekezaji kutoka Falme za Kiarabu limetenga paundi milioni 70 kuhakikisha pambano hilo linachezwa Dubai.
Baada ya miaka mingi ya kukwepana, huenda pambano hilo likafanyika May mwakani.
Mapambano mengi maarufu ya ndodi hata ya Mayweather yamekuwa yakifanyika jijini Las Vegas na ni mapambano machache ya aina hiyo yamekuwa yakifanyika nje ya Marekani.
Miaka 40 iliyopita, Muhammad Ali na George Foreman waligana nchini Zaire na mwaka 2001 Hasim Rahman alimtwanga Lennox Lewis nchini Afrika Kusini.
Chanzo: Daily Mail