Picha/Video: Nay wa Mitego aonesha ‘baadhi’ ya mali zake zenye thamani ya zaidi ya milioni 200
Rapper kutoka Manzese Nay wa Mitego ameamua kuonesha mali anazomiliki ikiwemo nyumba yake mpya pamoja na gari zenye thamani ya zaidi shilingi milioni 200.
Siwema akilia kwa uchungu baada ya kuona nyumba mpya ya mume wake
Akizungumza na Bongo5 jana akiwa nyumbani kwake Kimara Korogwe, Nay amesema imefikwa wakati wa kuonyesha baadhi ya mali zake anazomiliki. “Gari yangu mpya Nissan Murano nimenunua milioni 36, ni gari ambayo naipenda sana ,dream car yangu kwenye maisha yangu ni Murano , ninaweza nikabadilisha nikawa na gari nyingine, pia mimi napenda nyumba nzuri ,napenda kuishi kwenye nyumba nzuri, nina nyumba tatu, hii hapa ambayo nahamia kesho ina thamani ya shilingi milioni 170 kila kitu, lakini inaweza ikawa zaidi ya milioni 170 kwasababu kuna vitu vingine huwa sivipigii hesabu,” alisema.