Habari
Rais Magufuli aridhia ombi la kustaafu kwa Jaji wa Mahakama Kuu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli ameridhia maombi ya kustaafu mapema kwa jaji Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Prof. John Eudes Ruhangisa.
Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa Rais ameridhia maombi ya kustaafu mapema kwa jaji huyo kuanzia jana.
Jaji Ruhangisa alikuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania kanda ya Shinyanga.
Taarifa kamili hii hapa:
Na Emmy Mwaipopo