Habari
Rasmi: Mikel Arteta atangazwa kuwa kocha mpya Arsenal
Arsenal imemteua, Mikel Arteta kuwa kocha wao mpya kwa kandarasi ya muda wa miaka mitatu na na nusu.
Arteta anaondoka Manchester City akiwa kama kocha msaidizi na ambapo kwa sasa anakwenda kuchukua mikoba ya Unai Emery aliyetimuliwa kazi mwezi uliyopita.
Ljungberg ameiyongoza kwa muda Arsenal na kutoka sare mbili, akifungwa michezo miwili na kushinda mara moja.
https://www.instagram.com/p/B6TBKwBp2kI/