Michezo

Madrid walivyosherehekea na kombe la UEFA Hispania, Ronaldo afanyiwa sapraizi (picha+video)

Mabingwa wapya barani Ulaya, Real Madrid usiku wa kuamkia leo Mei 28 wamefanya sherehe kubwa ya kuwaonesha mashabiki wao Kombe kwenye uwanja wa Santiago Bernabeu jijini Madrid nchini Hispania.

Kabla ya Sherehe hizo jana mchana wabingwa hao walitembeza kombe la UEFA kwenye viunga vya jiji la Madrid wakiwa kwenye gari maalumu la wazi.

Kilichosisimua zaidi wakati wa sherehe hizo ni pale mshambuliaji wa klabu hiyo, Cristiano Ronaldo aliposimama na kutoa hotuba fupi ambayo hata kabla ya kumaliza hotuba hiyo wachezaji wenzake na mashabiki walimkatiza kwa kuimba wimbo uliokuwa unasikika kwa maneno ya “Ronaldo Stay, Ronaldo Stay”. Tazama video na picha za matukio yote.

https://youtu.be/okfDiuZwfLs

 

 

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents