Cristiano Ronaldo amedai kuwa Ligi Kuu ya Saudia (Saudi Pro League) ni bora zaidi kuliko ile ya Marekani (MLS) ambayo mshindani wake Lionel Messi amejiunga nayo kupitia Klabu ya Inter Miami.
Kauli ya Ronaldo imekuja siku moja tu baada ya Messi kutambulishwa timu ya Inter Miami inayoshiriki Ligi ya Marekani.
‘Nina uhakika kwa asilimia 100 sitarejea katika klabu yoyote ya Ulaya. Nilifungua njia kwa ligi ya Saudia na sasa wachezaji wote wanakuja hapa.”
Anaandika Hamza Fumo (@fumo255)