Burudani
Terrence J atua Dar, kesho atakuwa Slipway kugawa kitabu chake
Mtangazaji wa E! Entetainment TV ya Marekani Terrence J ameingia Dar es Salaam usiku wa july 10 ikiwa ni ahadi aliyoitoa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete ya kuwaleta wadau wa muziki ili kubadilishana mawazo na wasanii pamoja na wadau wamuziki wa Tanzania.
Terrence J kesho (july 12) saa 8:00 mchana atakuwa katika duka la A Novel Idea iliopo Slipway, Msasani, ambapo ataendesha kliniki ya kugawa bure kitabu chake cha “The Wealth of My Mother’s Wisdom” kwa watu 100 wa kwanza. Hivi vitabu vitasainiwa na Terrence J.
Pia kuanzia saa 2:00 usiku atakuwa katika usiku wa red carpet event ndani ya ukumbi wa Mlimani City ambapo ataonyesha filamu yake ya “Think like a man too” huku host ya show hiyo akiwa ni mwenyewe.