Burudani
Throwback Music: Ferooz – Umeniponza (Audio)
Ferooz ni miongoni mwa wasanii waliokuwa wakiunda kundi la Daz Nundaz lililotamba kwenye muziki wa Bongo Flava kitambo sana. Wasanii wengine waliounda kundi hilo walikuwa pamoja na Daz Baba, La Rhumba na Sajo.
Pamoja na kutengeneza hits zao kama kundi zikiwemo ‘Kamanda’ na ‘Barua’, Ferooz na Daz Baba waliweza kufanikiwa pia kama wasanii wanaojitegemea.
Ferooz alifanya vizuri sana na ‘Starehe’ aliyomshirikisha Profesa Jay lakini wimbo wake wa taratibu ‘Umeniponza’ ni moja ya nyimbo classic na zenye hisia zaidi kuwahi kufanywa Tanzania. Usikilize hapo juu.