Habari
VIDEO: Inawezekana wengine wamekufa kwa kukosa ajira, unawabeba kwenye magari yako kwenda kuwazika – Rais Magufuli
”Na ndiyo maana leo nakupongeza sana Mhe. Rostam kweli nakupongeza kwa sababu ndugu yako Mbunge wa hapa ameshindwa kuendesha viwanda viwili hapa, na mimi huwa ni mkweli nazungumzaga kwa uwazi ndugu Abood alichukua viwanda viwili vikubwa cha Canvas na Moproco, kiwanda cha Moproco kilikuwa kinahusika na Cooking Oil, mafuta …… mbunge wetu na mimi nakusema hadharani sikufichi ukapewa hivyo viwanda tangu mwaka 96 mpaka mwaka jana walipokunyang’anya miaka 24, kwa hiyo ukawanyima ajira hata wapiga kura wako, kwahiyo inawezekana wengine wamekufa kwa kukosa ajira lakini ikawa unawabeba kwenye magari yako kwenda kuwazika hongera kwa kuwazika, huu ndiyo ukweli na mimi nitabaki sikuzote kuzunguma ukweli,”- Rais Magufuli